Baba mzazi wa mwanamuziki huyo, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Abdul Jumaa ‘Baba D’.
MSHTUKO! Baada ya hivi karibuni staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kupata mtoto wa kike, Latifah Nasibu ‘Princes Tiffah’ kupitia kwa mwandani wake, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’, baba mzazi wa mwanamuziki huyo, Abdul Jumaa ‘Baba D’ amekataliwa kumuona mjukuu wake huyo, Risasi Mchanganyiko lina habari kamili.
Kwa mujibu wa baba Diamond, baada ya Tiffah kuzaliwa Agosti 6, mwaka huu, mama mzazi wa nyota huyo, Sanura Kassim a.k.a Sandra alimpigia simu mzazi mwenzake huyo na kumjuza kwamba wamepata mjukuu, jambo ambalo walilifurahia kwa pamoja. 


0 comments Blogger 0 Facebook

Post a Comment

 
Heka Heka Zangu © 2015. All Rights Reserved. Share on mfaume.com. Powered by mfaume.com
Top