Katika kila mwanadamu anayejitambua lazima atakuwa na kitu kinaitwa “core principles.” Yani hizi ni kanuni kuu za msingi wa maisha yako ambazo zinakupa ‘identity’ ya wewe ni nani au mtu wa namna gani! Hizi si misingi au miiko uliyo jiwekea tuu kwasababu ya kujifurahisha, hapana! Ni misingi na miiko unayoiyamini na hukotayari kuisimamia bila kutetereka kwa gharama yoyote ile. Haijalishi hata kama watu wote watakuona wewe ni mtu wa ajabu, lakini kwako itakuwa salama rohoni mwako kwasababu hizo ni principle zako za maisha umejiwekea, unaiyamini, na hupo teyari kuitetea mpaka kufa! “A man who stand for nothing will fall for anything”-Malcolm X. Mtu ambaye hana msingi au miiko katika maisha yake ni mtu ambaye hajitambu na wala hajui dhamani yake! Nandiyo maana watu kama hawa wanaweza leo wakasimama na kutowa kauli kali kwenye kadamunasi kama “over my dead body” lakini kesho bila aibu wala soni usoni akafanya kile kile ambacho alikanusha kuwa hawezi kufanya unless it’s over his / her dead body! SMH!
Misingi na miiko mbayo mtu anajiwekea ndizo zimefanya baadhi ya watu wameitwa “Pioneers” wa kitu fulani. Iwe kwenye siasa, imani za kidini, au mambo ya kijamii kuna pioneers wa aina mbali mbali na watu tunawangalia kama kioo au role-model! Watu wanao jitambua pamoja na pioneers watakwambia kunavitu ambavyo siwezi ku-compromise hata kidogo, kwa mfano wapo wengi atakwambia mie hata sikumoja siwezi ku-compromise my core-principles; na moja ya misingi yao nikujali sana UTU NA HESHIMA yao! Sikuzote utu na heshima yao vitakuja kwanza kabla ya kitu kingine chochote kile (his / her dignity and respect will always comes first no matter what!). Mtu anaweza kuwa yupo teyari kuacha kila kitu kipotee hata kama anaonewa ili kulinda utu na heshima yake. Inaweza ika-sound crazy to other people lakini hii ndiyo miiko au misingi yake aliyojiwekea na yupoteyari kuisimaimia kwa gharama yoyote ile.

0 comments Blogger 0 Facebook

Post a Comment

 
Heka Heka Zangu © 2015. All Rights Reserved. Share on mfaume.com. Powered by mfaume.com
Top